Mradi wa ujenzi wa Kituo cha Huduma za Pamoja Mpakani (OSBP) mwa Tanzania na Malawi eneo la Kasumulu umefikia asilimia 67.1 na unatarajiwa kukamilika mwezi ujao.
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Godfrey Kasekenya,ameyasema hayo baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa kituo hicho unaojengwa kwa awamu tatu kwa gharama ya zaidi ya Sh bilioni 26. Unaojengwa na Mkandarasi China Geo Engineering Corporation.
“Nitoe wito kwa mhandisi mshauri kuusimiamia mradi huu kikamilifu ili ukamililike kama ulivyopangwa kulingana na mkataba,”
Alisema hadi sasa Mkandarasi hajawasilisha changamoto zozote ambazo zinaweza kumkwamisha asimalize mradi huo kwa wakati, hivyo ni mategemeo yao kuwa kila kitu kitakwenda kama kilivyo pangwa.