Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kisumu: Watu 13 wafariki dunia baada ya tanka kuanguka na kulipuka

2853f79d83306721 Kisumu: Watu 13 wafariki dunia baada ya tanka kuanguka na kulipuka

Sun, 18 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Tanka hiyo iligongana na lori nyingine na kuanguka huku ikimwaga mafuata yaliyowavutia wakazi na kukimbia kuchotaDakika chache baadaye ililipuka na waliokuwepo wakaangukiwa na ndizi za moto uliokuwa na hasiraOCPD wa eneo hilo alisema moto huo ulikuwa mkubwa na ulichukua masaa kadhaa kuzimwa na kitengo cha wazima moto kaunti hiyoWatu kumi na watatu walipoteza maisha yao Jumamosi Julai 17 baada ya ajali iliyohusisha lori la mafuta.

Duru zinaarifu tanka hiyo ya mafuta ilianguka katika eneo la Malanga kwenye barabara ya Kisumu-Busia na wakazi wakakimbia kuchota mafuta.

Kamanda wa polisi kaunti ndogo ya Gem Charles Chacha, alisema ajali hiyo itafanyika saa nne kwenye kijiji hicho.

Alisema lori hiyo iligongana na nyingine ya maziwa baada wa dereva wake kupoteza udhibiti na mwelekeo.

Habari Nyingine: Kangogo Alisafiri Mombasa Kumuua Aliyekuwa Mumewe Lakini Akamsamehe

"Trela hiyo iligongana na lori hiyo upande wa kulia. Kutokana na hilo, ilianguka na kuanza kumwaga mafuta," aliaambia wanahabari.



Read also

Kaburi Huficha Mengi: Maswali Yaibuka Kuhusu Kifo cha Caroline Kangogo

Ni hapo ambapo wananchi walikimbia na kuanza kuchota mafuta kabla ya moto mkubwa kulipuka na kuwachoma.

Alisema miili kumi na miwili ilichomeka hadi kuwa makaa katika mkasa huo huku akionya wananchi kujiepusha na visa kama hivyo.



"Tulihesabu miili kumi na wili katika eneo la mkasa. Watu wengine kumi na mmoja waliokolewa na kukimbizwa hospitalini," alisema Chacha.

Baada iliibuka kuwa kulikuwa na maafa zaidi na idadi ya walioangamia ikafikia watu kumi na watatu.

"Kilikuwa kisa cha kuhuzunisha sana kwani moto huo ulichukua masaa matatu kabla ya kitengo cha wazima moto kufaulu kuuzima," alisema kamanda huyo wa polisi.

Wakenya wamekosa kujipa funzo kutokana na mikasa ya moto inayohusisha trela za mafuta na wao hukimbilia kuchota mafuta baada ya kuona tanka imeanguka.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.



Read also

Magazeti Ijumaa: Babu wa Miaka 93 Afunga Ndoa na Kipusa wa Miaka19

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke