Serikali ya Rwanda imethibitisha kuwa visa sita vya aina mpya ya virusi vya corona aina ya Omicron.
Imesema visa hivyo viligundulika katika sampuli zilizokusanywa kutika kwa wasafiri pamoja na watu wengine waliokutana na wasafiri hao, kulingana na taarifa ya wizara ya afya.
Imesisitiza haja ya watu wote wenye umri wa miaka 12 na zaidi kupata chanjo kamili na wale wenye umri wa miaka 18 na zaidi kuangalia uwezekano wa kupata chanjo ya kuboresha chanjo za awali.
Tangazo hilo limetolewa kwenye ukurasa wa Twitter
The Ministry of Health has confirmed cases of the #Omicron variant in Rwanda through genomic sequencing of samples collected from travelers and their contacts. pic.twitter.com/Q3rNtlz06p
— Ministry of Health | Rwanda (@RwandaHealth) December 14, 2021
Rwanda imekwishawachanga asilimia 40 ya watu wake na hivi karibuni ilianza kutoa chanjo ya kuimarisha kinga ya chanjo za awali.