Kiongozi wa upinzani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) anayeishi uhamishoni Corneille Nangaa ametangaza kuunda Kitengo cha Kisiasa cha Kijeshi kitakachokuwa mshirika wa kundi la Waasi wa M23 na makundi mengine yenye silaha ili 'kuiokoa nchi'
Hali kisiasa na usalama Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imekuwa na wasi wasi mkubwa kuelekea uchaguzi wa Desemba 20 mwaka huu
Nangaa ambaye ni Mkuu wa zamani wa Tume ya Uchaguzi ametoa tangazo hilo akiwa Nairobi Jijini Nairobi, nchini Kenya ambapo kwenye kufikisha ujumbe huo alikuwa sambamba na Bertrand Bisimwa “rais” wa kundi la M23 kwenye Hoteli moja katika mji mkuu wa Kenya
Vitendo vyao vimesababisha zaidi ya watu milioni moja kukimbia nyumba zao ambapo kulingana na Umoja wa Mataifa Hali ya wasi wasi imeongezeka zaidi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa wiki ijayo