Kiongozi wa upinzani nchini Benin Reckya Madougou amehukumiwa kifungo cha miaka 20 gerezani mara baada ya kukutwa na hatia ya kuhusika kwenye shughuli za ugaidi.
Mahakama hiyo ya Uhujumu Uchumi na Ugaidi iliyoanzisha mwaka 2016 na Rais wa nchi hiyo Patrice Talon inatajwa kutumika kama fimbo ka wale wote wanaokosoa utawala wa Rais huyo
Reckya ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Haki nchini humo amehukumiwa kwa makosa hayo mara baada ya kesi hiyo kusikilizwa kwa zaidi ya saa 20 siku ya uhukumu hiyo.
Kelele na minong'ono mingi ni juu ya utendai wa haki unaofikiwa na Mahakama hiyo huku wengi wakidai kuwa inatumiwa sana na Mamlaka kama fimbo kwa wapinzani.