Kiongozi mwandamizi wa Sudan Mohamed Hamdan Dagalo anakwenda Ethiopia leo, kwa ziara ya nadra ya afisa wa serikali ya Khartoum tangu mataifa hayo mawili yalipotumbukia kwenye mivutano kuhusu mipaka.
Shirika la habari la Sudan SUNA limeripoti kuwa Dagalo, ambaye ni kiongozi wa pili wa ngazi ya juu katika Baraza la Tawala la kijeshi nchini Sudan, atakuwa Ethiopia kwa siku mbili ili kukutana na maafisa kadhaa wa nchi hiyo.
Afisa huyo wa Sudan ni mkuu wa kikosi maalumu chenye nguvu cha RDF, kinachoogopwa kutokana na rikodi yake ya vitendo vya ukatili hasa katika jimbo la magharibi la Darfur. Mahusiano kati ya Sudan na Ethiopia yamezorota kutokana na mzozo juu ya eneo la mpaka linalozozaniwa la Al-Fashaqa Magharibi ambalo kila upande linadai haki ya umiliki.