Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kimbunga Hidaya: Mvua kunyesha pwani ya Kenya

Kimbungaaaa (5).jpeg Kimbunga Hidaya: Mvua kunyesha pwani ya Kenya

Sun, 5 May 2024 Chanzo: Bbc

Idara ya hali ya hewa ya Kenya sasa inasema kimbunga Hidaya kilichotarajiwa kimepoteza nguvu zake baada ya kutua nchini Tanzania.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Huduma za Hali ya Hewa David Gikungu amesema licha ya kudhoofika kwa kimbunga hicho, mvua bado inatarajiwa kunyesha katika maeneo ya pwani ya Kenya.

Gikungu amesema kaunti za Kwale, Mombasa, Kilifi na Lamu huenda zikakumbwa na mvua za wastani hadi nyingi.

“Kufuatia kutua kwa kimbunga hicho katika kisiwa cha Mafia siku ya Jumamosi Mei 4, 2024, kimbunga Hidaya kilipoteza nguvu kabisa, mabaki ya mawingu ya mvua yaliyoambatana na kimbunga hicho yameonekana kupungua na kusambaa katika maeneo mbalimbali ya ukanda wa kusini mwa Tanzania. , kama ilivyothibitishwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania," Gikungu alisema.

Alisema mvua hiyo ya wastani hadi kubwa huenda ikaendelea kunyesha ndani ya siku ya Jumatatu na Jumanne huku ikiambatana na upepo mkali.

Mkurugenzi huyo alisema upepo huo mkali unatarajiwa kupiga huku mawimbi makubwa ya bahari yakiweza kupanda urefu wa mita mbili.

Gikungu amesema maeneo mengine ya nchi pia yanapaswa kutarajia mvua za wastani za mara kwa mara kati ya milimita tano hadi 20 hadi mvua kubwa za kati ya 20-50mm.

Chanzo: Bbc