Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kijogoo afunzwa adabu kwa kuchovya asali ya mke wa wenyewe

87bbf0488c2b38f1 Kijogoo afunzwa adabu kwa kuchovya asali ya mke wa wenyewe

Sun, 18 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Jamaa aliyemtembelea mpango wa kando kushiriki ufuska alilazimika kubaki na njaa baada ya mume wa mwanamke kurejea na kufunga safari naye huku kijogoo akisalia kujificha mvunguni mwa kitanda.

Semasema zinaarifu kwamba jamaa alikuwa na mazoea ya kupakua asali katika mizinga ya wenyewe huku akiapa kutokoma tabia hiyo licha ya kuonywa na wengi.

“Jamani nawaapia, niliyoonja si asali ya kawaida. Husemwa mzinga wa wenyewe kudondosha asali tamu na hili nimeamini. Siwezi kuiacha hata mauti yakinikodolea macho,” polo aliwaeleza rafikize mtaani kulingana na Taifa Leo.

“Mke wa mtu ni kifo rafiki yangu. Tunakupenda sana na hatutaki kuhudhuria mazishi yako hivi karibuni. Achana na mke wa mtu!” mmojawa marafiki zake wa karibu alimuonya lakini jamaa alitia masikio nta na kumpuuza.

Siku ya kisanga, jamaa aliandaliwa ugali kwa kitoweo cha kuku lakini kabla hata anawe mkono na kukivamia chakula mwenye boma akaingia ghafla.

Inasemekana, mke alilazimika kumsukuma mvunguni mwa kitanda kisha akufungua mlango kumkaribisha mumewe.

“Switi twaondoka sasa hivi, kuna mahali nataka twende tutarudi siku tatu baadaye,” mume alimwagiza mkewe.

“Lo! Safari ya wapi jamaa hivi ghafla?” mama wa nyumba aliuliza kwa mshangao.

“Usijali switi. Valia nguo maridadi tuondoke,” mume alimharakisha kisura.

Inasemekana wawili hao waliondoka huku mume akifunga milango yote. Jamaa alibaki amezubaa akawa hajui afanye nini.

Siku ya kwanza njaa ilipomlemea ilibidi ale sima waliyokuwa wamepika na mpango wake wa kando, siku ya pili akala sima kwa avocado nayo ilipofika siku ya tatu akawa hana chakula.

Duru zinaarifu kuwa siku ya nne alipolemewa ilibidi apige mayowe asaidiwe na majirani kuvunja mlango ili wamuokoe.

Hata hivyo, waliingia na kumfunga kamba kisha wakampigia simu mwenye nyumba ili kumfunza adabu.

“Mumefanya makosa kumuokoa. Nilimwaccha humu makusudi nimfunze adabu. Siku nyingine nikikushika hapa kwangu nitakunyonyoa. Ondoka haraka!” jamaa alifukuzwa.

Tangu siku hiyo, lofa alishika adabu akawakoma wake za wenyewe kabisa.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke