Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kijana mwenye umri wa miaka 21 akamatwa na DCI kwa kudukua data za IEBC

5d0fab174d0446c5 Kijana mwenye umri wa miaka 21 akamatwa na DCI kwa kudukua data za IEBC

Mon, 19 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mshukiwa huyo kwa jina Kiprop anadaiwa kudukuwa data za IEBC na kuchukua habari muhimu za wapiga kura 61,617Mshukiwa huyo alikamatwa baada ya kuibia ajenti wa simu kiasi cha pesa zisizojulikana mjini Juja, akitumia teknolojia ya hali ya juu na data za IEBCAlikamatwa na begi iliyojaa kadi za simu za Safaricom, Airtel na Telcom

Makachero kutoka Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) wamemkamata mshukiwa kuhusiana na udukuzi wa data ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).

Mshukiwa huyo kwa jina Kiprop anadaiwa kudukuwa data za IEBC na kuchukua habari muhimu za wapiga kura 61,617 kutoka kaunti moja ya magharibi mwa Kenya.

Kiprop alikamatwa Ijumaaa, Julai 16, akiwa na mabegi yaliyojaa kadi za simu ambazo amekuwa akizitumia kufanya utapeli.



Read also

"Barikiwa": DP Ruto Afurahishwa na Mfuasi Wake Kutoka Elburgon Anayehubiri Injili Yake

Mshukiwa huyo alikamatwa baada ya kuibia ajenti wa simu kiasi cha pesa zisizojulikana mjini Juja, akitumia teknolojia ya hali ya juu na data alizopata kuendesha utapeli wa simu.

DCI iliongezea kuwa tapeli huyo aliyekuwa anajifanya mhudumu wa Mpesa alimpigia ajenti huyo na kumvizia kufinya nambari kadhaa zisojulikana.

“Kabla ya ajenti kujua alikuwa anatepeliwa, tayari alikuwa amepoteza pesa kwenye akaunti yake," ilisem DCI.

Pesa hizo zilitumwa katika moja ya akaunti ya Mpesa ya kadi za wizi kabla ya kuwekwa kwenye akaunti ya benki ya Cooperative.

“Kukamatwa kwake ni kufuatia ushirikiano kati ya makachero na wapelelezi wa Safaricom baada ya mshukiwa kumuibia ajenti wa Mpesa kiasi ya pesa zisizojulikna,” DCI ilisema.

Majina ya wapiga kura, nambari zao za vitambulisho, siku za kuzaliwa ni miongoni mwa habari alizopatwa nayo.

Kulingana na DCI, washukiwa huwapigia simu waathiriwa kupitia nambari tofauti za simu wakidai ni wahudumu wa wateja wa kampuni hiyo ya simu.



Washukiwa huchukuwa taarifa zote za waathiriwa mtandaoni baada ya kubadilisha kadi zao za simu.

Mshukiwa mwenye umri wa miaka 21, anaripotiwa kuwa aliwahi kufanya kazi katika moja ya kampuni za mawasiliano nchini.

Alikamatwa na begi iliyojaa kadi za simu za Safaricom, Airtel na Telcom.

Mshukiwa huyo alikamatwa eneo la Juja na makachero kutoka Kitengo cha Kuchunguza Uhalifu wakishirikiana na kikosi cha Safaricom cha upelelezi wa utapeli na maafisa wa usalama wa Chuo Kikuu cha Jomo Kenyatta.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke