Mwili wa kijana mdogo umegunduliwa katika jengo ambalo halijakamilika huko Buokrom - Quarry, kitongoji cha Kumasi katika Mkoa wa Ashanti.
Mwili wa kijana huyo aliyetambulika kwa jina la Kwabena Atuahene, ulikutwa kwenye jengo hilo ambalo halijakamilika ukiwa umeshaharibika siku chache baada ya kufariki dunia.
Kisa hicho kimezua hofu miongoni mwa wakazi katika eneo hilo huku wengi wakishukiwa kuwa na mchezo mchafu katika kifo cha kijana huyo.
Shahidi katika mahojiano na OTEC News’ Kwame Agyenim Boateng alisema kisa hicho kilikuja kujulikana mnamo Jumatatu Julai 26, mwendo wa saa 4:00 usiku kutokana na harufu kali iliyokuwa ikitoka kwenye mwili huo uliokuwa ukioza.
"Fundi Seremala ambaye amepewa jukumu la kufanya kazi katika jengo hilo, aliona mwili Jumatatu."
"Tuliita polisi mara moja kutusaidia katika hali hii kwa sababu wengi wetu tulikuwa na hofu," mkazi mmoja alisema.
Mwili wa marehemu kulingana na wakazi wa eneo hilo, umefikishwa hospitalini na polisi katika eneo hilo.