Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kijana aliyenaswa kwenye video akimpiga polisi wa Kenya akamatwa

Kijana Aliyenaswa Kwenye Video Akimpiga Polisi Wa Kenya Akamatwa Kijana aliyenaswa kwenye video akimpiga polisi wa Kenya akamatwa

Mon, 3 Jun 2024 Chanzo: Bbc

Polisi nchini Kenya wamemkamata dereva wa gari mwenye umri wa miaka 19 ambaye alirekodiwa akimpiga polisi wa trafiki akiwa kazini mjini Nairobi.

Katika video ambayo imekuwa ikisambazwa sana, kijana huyo anaonekana akimshambulia polisi huyo kwa makonde na mateke ya kichwa hata baada ya afisa huyo kuanguka chini.

Dereva huyo alitoroka baada ya watu wengine kuingilia kati kumsaidia afisa huyo.

Shambulio hilo la kushtukiza limezua hisia nadra ya huruma kwa polisi, ambao wana sifa ya ukatili na ulaji riushwa.

Ripoti ya polisi ilisema mtu huyo alisimamishwa awali baada ya kugeuza gari kwenye barabara yenye mshughuli nyingi, na kuwazuia madereva wengine kuendelea na safari zao.

Ilisema kuwa afisa wa trafiki, Patrick Ogendo, aliingia ndani ya gari hilo na kumwagiza aendeshe hadi kituo cha polisi kilicho karibu.

Wakiwa njiani, "dereva alisimama ghafla na kuchomoa upanga chini ya kiti".

"Afisa huyo aliruka nje ya gari kwa usalama wake ndipo dereva akaanza kumpiga makonde na mateke," taarifa hiyo iliongeza.

Polisi huyo alipata huduma ya kwanza katika kituo cha afya kilicho karibu na kisha kupelekwa hospitali kwa matibabu.

Mtu anayedaiwa kuwa mshirika wa mshukiwa huyo alikamatwa katika eneo la tukio na maafisa wa polisi waliokuwa wakifanya msako wa kumtafuta mtu aliyefanya shambulizi hilo, ilisema taarifa hiyo.

Shambulio hilo limelaaniwa vikali, huku wengine wakielezea shambulio hilo kuwa halikubaliki.

“Unamshambulia vipi afisa wa polisi aliyevalia sare kwa njia hii?” akauliza Robert Alai, mjumbe wa bunge la kaunti ya Nairobi.“Hili halikubaliki kabisa.

Hatufai kuruhusu maafisa wetu wa polisi waliovalia sare kudhalilishwa hadi kiwango hiki,” akasema Mike Sonko, gavana wa zamani wa Nairobi.

Mshukiwa aliripotiwa kukamatwa katika makazi yake viungani mwa mkuu baadaye Jumapili jioni.

Mkuu wa trafiki wa Nairobi Vitalis Otieno aliambia vyombo vya habari kuwa atashtakiwa kwa makosa kadhaa ikiwemo jaribio la mauaji.

Chanzo: Bbc