Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kidato cha Nne Auawa Akigombania Mwanamke Baa

ER Mauaji

Tue, 12 Oct 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya upili ya Kapsinendet kaunti ya Bomet nchini Kenya amefariki dunia baada ya kudungwa kisu na mwanaume mmoja wakiwa kwenye baa wakigombania mwanamke.

Inaelezwa kwamba wawili hao walikuwa wakizozania mwanamke mmoja kwenye baa kabla ya mshukiwa kuchukua kisu na kumdunga mwanafunzi huyo.

Kwa mujibu wa taarifa za Citizen, mwanaume huyo ambaye hajatambulika anadaiwa kumdunga mwathiriwa kisu mara mbili kwenye shingo kabla ya kutoroka.

Mwanamke aliyekuwa akipiganiwa alitoroka eneo la tukio baada ya kushindwa kuwatuliza wanaume hao. Mwanamke huyo anasemekana alihamia eneo la Siongiroi kutoka Sotik hivi karibuni.

Maafisa wa polisi walifanikiwa kumkamaata mshukiwa na wanamzuilia katika kituo cha Chebunyo kaunti ya Bomet huku uchunguzi ukianzishwa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live