Sat, 23 Apr 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliyekuaa Rais wa tatu wa jamuhuri ya Kenya Emilio Stanley Mwai Kibaki atazikwa tarehe 30 April mwaka huu 2022 nyumbani kwake kaunti ya Nyeri.
Mwenyekiti wa Kamati ya kitaifa ya mazishi ya kiserikali amesema kuwa kutakua ibaada ya kimataifa ya kuuaga mwili wa marehemu Rais Kibaki katika Uwanja wa michezo wa Kasarani mnamo ijumaa tarehe 29th aprili mwaka huu.
Aidha wananchi na viongozi watapewa muda wa siku tatu wa kutoa heshima zao katika majengo ya bunge jijini Nairobi ambako mwili wa marehemu utalazwa kwa siku tatu kuanzia jumatatu tarehe 25 aprili hadi Jumatano tarehe 27 juma hili.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live