Katazo hilo linakuja ikiwa ni masaa chini ya 24 yamesalia kwa Mahakama Kuu kutoa uamuzi wa mwisho kuhusu Matokeo ya Rais ambayo yaliwekewa Pingamizi na Mgombea wa Azimio, Raila Odinga.
Katika taarifa yake Jeshi la Huduma za Polisi (NPS) pia limezuia matumizi ya Barabara zote zinazoelekea katika Mahakama Kuu ambazo zitafungwa ili kuepusha mikusanyiko kwenye jengo hilo wakati wa kutolewa uamuzi wa Majaji
Ijumaa Septemba 2,2022 Mahakama Kuu ilihitimisha kusikiliza Pingamizi hilo na inatarajiwa kurejea tena Jumatatu Sept. 5,2022 kwa ajili kutoa uamuzi wa kamati ya Majaji 7 inayoongozwa na Jaji Mkuu Martha Koome.