Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kenyatta awashauri Wakenya kula pesa za DP Ruto, lakini wasimpe kura 2022

C209fd09a68aae83 Kenyatta awashauri Wakenya kula pesa za DP Ruto, lakini wasimpe kura 2022

Wed, 20 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais Uhuru Kenyatta amewahimiza wakazi Mlima Kenya wawachunguze wagombea wote wa urais kabla kuwapigia kura. Uhuru amewatahadharisha wananchi pia dhidi ya kununuliwa na wanasiasa akidai kwamba mwishowe ni wao wataumia.

Uhuru amekuwa akionyesha dalili za kumuidhinisha Raila kumrithi 2022Rais Uhuru Kenyatta amewashauri wakazi wa eneo la Mlima Kenya kuchukua pesa wanazopewa na Naibu Rais William Ruto lakini wawe chonjo wasidanyanganywe na ahadi za uwongo.

Akizungumza akiwa Gichugu kaunti ya Kirinya Jumatatu, Oktoba 18, Rais Uhuru aliwahimiza wakazi wawachunguze kwa kina wagombea wote wa urais ambao wanatazamia kumridhi kabla kufanya uamuzi.

Akionekana kumshambulia naibu wake William Ruto, Uhuru aliwashauri wakazi hasa wa eneo la Mlima Kenya wachukue pesa kutoka kwa wanasiasa wanaozunguka wakipena kwenye kampeni lakini watakapoenda debeni wachague viongozi ambao watawahudumia inavyotakikana.

" Lakini wale ambao wanatafuta kura zenu na wanaona wana pesa za kuwapatia, chukua lakini waambie wazingatie na wafikirie kwa undani kabla ya kutoa ahadi ambazo zingine huenda hawatatimiza,"Uhuru alisema.

Uhuru ambaye amekuwa akionyesha dalili za kumuidhinisha Raila Odinga kama mrithi wake, alisema kwamba wakazi wa eneo la Mlima Kenya wanapaswa kuchagua viongozi wenyewe sio kulazimishiwa viongozi.

Rais aliwatahadharisha wakazi pia dhidi ya kununuliwa na wanasiasa akidai kwamba mwishowe ni wao wataumia iwapo hawatafanya uamuzi dhabiti.

" Kaeni macho, msije mkanunuliwa na peni mbili, epuka wale wanaozungumza vibaya kuhusu viongozi wenu, msije mkajutia baadaye,"Uhuru aliongezea.

" Msikubali kupotoshwa, wengi wao wanatumia maneno matamu lakini hayazai matunda, mwishowe mwananchi wa kawaida ndiye anaumia na wao wanajinufaisha,"Uhuru aliongezea.

Wanasiasa kadhaa wamekuwa wakizunguka sehemu mbali mbali wakifanya kampeni za kujipigia debe.

Uhuru aatarajiwa kustaafu mwaka wa 2022 baada ya kuhudumu kama Rais kwa mihula miwili, wanasiasa kadhaa akiwemo Raila na naibu wake William Ruto wametangaza kukiwania kiti hicho.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke