Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kenyatta afurahia jumbe alizotumiwa na Wakenya siku yake ya kuzaliwa

7afe3c38379bbf29 Kenyatta afurahia jumbe alizotumiwa na Wakenya siku yake ya kuzaliwa

Wed, 27 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais Uhuru Kenyatta amesherehekea siku yake ya kuzaliwa Jumanne, Oktoba 26 huku akipokea salama za heri kutoka kwa Naibu Rais wake William Ruto, Wakenya pia mitandaoni walimtumia jumbe za heri njema baada ya kutimiza miaka 60.

Kupitia kwenye taarifa rasmi kutoka Ikulu, Rais amewashukuru Wakenya kwa jumla kwa jumbe tamu alizopokeaRais Uhuru Kenyatta amewashukuru Wakenya wote waliofurika kwenye mitandao ya kijamii kumtakia heri njema siku yake ya kuzaliwa.

Uhuru ambaye alitimia umri wa miaka 60, siku ya Jumanne, Oktoba 26, alizaliwa Oktoba 26 mwaka wa 1961 akiwa mtoto wa Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Kenya, Mzee Jomo Kenyatta na Mama Ngina Kenyatta.

Hii hapa taarifa yake Rais ya shukurani kwa Wakenya;

"Mheshimiwa Rais Uhuru Kenyatta amepokea jumbe za heri njema kwa furaha na moyo mkunjufu alipokuwa akiadhimisha miaka 60 hapo jana. Rais amemshukuru kila mmoja ambaye alichukua fursa na muda wake kumtakia heri njema na anaomba kwamba Mungu azidi kuwabariki na kuwainua katika kila jambo," Taarifa ya Rais Kutoka Ikulu.

Miongoni mwa viongozi waliomtakia kila la heri Rais ni naibu wake William Ruto ambaye alikuwa na ujumbe huu;

"Tafadhali ungana nami kumtakia kiongozi wetu, rais, mheshimiwa Uhuru Kenyatta, siku njema ya kuzaliwa kwake, na kumwombea mafanikio anapoongoza taifa kuafiki ahadi kubwa zaidi,” alisema.

"Mungu akubariki na akuzidishie miaka mingi zaidi duniani ili upate kusherehekea bathidei nyingi hata zaidi," aliongezea Ruto.

Kwingineko, wakazi wa Homa Bay wakiongozwa na mwakilishi wa wanawake Gladys Wanga walisisimua mitandao ya kijamii baada ya video yao kusambaa ikiwaonyesha wakimuimbia nyimbo za sifa na kumtakia Rais maisha marefu yenye baraka.

Baadhi ya jumbe za Wakenya kwa Rais;

@Dianah Kamande:

" Heri njema siku yako ya kuzaliwa mheshimiwa Rais, Mungu akubariki sana, tunajivunia kama taifa kuwa na kiongozi kama wewe."

@Cate Kamande:

"Happy birthday Uhuru, ni baraka kuwa miaka 60, nakutakia miaka mingine mingi yenye baraka tele."

@Josephine Githaiga:

"Happy, happy birthday mheshimiwa Rais, Mungu na akupe neema mpya mwaka huu mpya na mingine mingi inayokuja."

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke