Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kenya yatia saini makubaliano ya biashara bila ushuru na EU

Kenya Yatia Saini Makubaliano Ya Biashara Bila Ushuru Na EU Kenya yatia saini makubaliano ya biashara bila ushuru na EU

Mon, 19 Jun 2023 Chanzo: Bbc

Kenya na Umoja wa Ulaya zimesaini mkataba wa kibiashara ambao ukishaidhinishwa, utaipa Kenya ufikiaji wa soko la EU bila kutozwa ushuru.

Mkataba huo unatarajiwa kuimarisha maendeleo ya kiuchumi ya Kenya, huku Rais William Ruto akisema "utachochea utengenezaji wa bidhaa nchini Kenya na usafirishaji wa bidhaa zilizokamilika, zilizoongezwa thamani nje ya Kenya".

Waziri wa Biashara Moses Kuria aliitaja hatua hiyo kuwa "wakati wa fahari" kwa nchi, baada ya kutia saini Mkataba wa Ushirikiano wa Kiuchumi wa EU-Kenya (EPA) na Kamishna wa Biashara wa EU Valdis Dombrovskis.

EU ni mojawapo ya soko kubwa la Kenya na inauza takribani moja ya tano ya mauzo yake yote huko - inasheheni bidhaa nyingi za kilimo ikiwa ni pamoja na mboga mboga, maua , chai na kahawa.

Kenya pia inatarajiwa kupunguza vikwazo kwa bidhaa za Umoja wa Ulaya hatua kwa hatua.

Taarifa ya EU ilibainisha kuwa haya yalikuwa makubaliano ya usawa, kwani inazingatia "mahitaji ya maendeleo ya Kenya kwa kuiruhusu muda mrefu kufungua soko lake".

Chanzo: Bbc