Tue, 9 Apr 2024
Chanzo: Bbc
Kenya imetangaza Jumatano, Aprili 10, 2024 kuwa siku ya mapumziko kuadhimisha Eid-Ul-Fitr.
"Katika kutekeleza mamlaka yaliyotolewa na kifungu cha 2 (1) cha Sheria ya Sikukuu za Umma, natangaza Jumatano, Aprili 10 2024, itakuwa sikukuu ya kuadhimisha Idd-ul-Fitr," Waziri wa Mambo ya Ndani nchini Kenya Kithure Kindiki alisema.
Eid-ul-Fitr ni sikukuu kwa Waislamu ambayo inaashiria mwisho wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan ambao ni wa tisa wa kalenda ya Kiislamu.
Sherehe hiyo huanza kwa sala maalum, inayojulikana kwa jina la Eid, inayoswaliwa mapema asubuhi baada ya kuonekana kwa mwezi.
Chanzo: Bbc