Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kenya yapokea shehena ya chanjo ya Covid-19

8f353d8fe6304a8eb1d2e017f08cc66a 660x400 Kenya yapokea shehena ya chanjo ya Covid-19

Thu, 4 Mar 2021 Chanzo: millardayo.com

Shehena ya chanjo ya Covid-19, dozi milioni 1.02 za Oxford-AstraZeneca imetua katika uwanja wa Jomo Kenyatta Jijini Nairobi nchini Kenya, ikitokea taifa la India.

Chanjo hizo zilizofika usiku wa kuamkia leo Machi 3, 2021, ni shehena ya kwanza kati ya chanjo milioni 3.56 zitakazopelekwa Kenya.

Aidha, taarifa kutoka Kenya zimeeleza kuwa chanjo hiyo itaanza kutolewa kesho kwa Wahudumu wa Afya, Walimu na walio na magonjwa mbalimbali.

Kwa upande wa viongozi wa nchi ambao ni Rais Uhuru Kenyatta, Naibu Rais William Ruto na kiongozi wa upinzani Raila Odinga wanatarajiwa kupewa chanjo hiyo siku ya Jumamosi, Machi 6, 2021.

FISI 22 WAUAWA, WAMEUA WATU WATANO, MAMA AMWAGA MACHOZI “LIFISI LIMEKULA MTOTO WANGU”

Chanzo: millardayo.com