Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kenya kuendeleza juhudi za kutokomeza ugonjwa Ukimwi

Kenya Kuendeleza Juhudi Za Kutokomeza Ugonjwa Ukimwi Kenya kuendeleza juhudi za kutokomeza ugonjwa Ukimwi

Thu, 30 Nov 2023 Chanzo: Voa

Serikali ya Marekani imetangaza kuwa itaendelea kuwa sehemu ya juhudi za ushirikiano katika kutokomeza kabisa ujonjwa wa UKIMWI.

Kupitia balozi wake jijini Nairobi, Meg Whitman, serikali ya Marekani imesema kuwa itaendelea kushirikiana na Kenya ili kudhibiti kabisa janga hilo na kulitokomeza tishio la VVU/UKIMWI kama afya ya umma.

Katika maadhimisho ya miaka 20 ya Mpango huo wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi unaojuliakana kama PEPFAR, rais William Ruto ameishukuru serikali ya Marekani na kueleza kuwa Kenya imepiga hatua za wazi na muhimu ambazo zimebadilisha hali ya taifa la Kenya kwa kuziwezesha jamii nyingi kujilinda dhidi ya makali ya virusi vya ukimwi.

Ruto anaeleza kuwa ushirikiano huu kupitia PEPFAR, umesababisha mabadiliko ya moja kwa moja, ya binafsi, yanayoonekana katika maisha na ustawi wa raia wa Kenya katika juhudi za kukomesha mateso, kupunguza idadi ya vifo na kurefusha maisha ya mamilioni ya wananchi wa Kenya ambao wamekuwa wakikabiliwa na hatari kubwa ya kifo na makovu ya kudumu yanayosababishwa na maambukizi ya virusi vya Ukimwi.

Chanzo: Voa