Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kenya kuchukua mkopo mwingine wa KSh780 bilioni kutoka Eurobond

7a54b4031b3a328c Kenya kuchukua mkopo mwingine wa KSh780 bilioni kutoka Eurobond

Thu, 8 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Kulingana na mpango wa mkopo ambao uliwasilishwa kwa IMF na Wizara ya Fedha, Kenya inapanga kukopa KSh 528 bilioni ambao una muda mrefu wa kulipa

- Mkopo mwingine wa KSh 253 bilioni ni wa kibiashara ambao una riba ya juu na kipindi kifupi cha kulipa

- IMF ilisema mpango huo unaruhusu Kenya kukopa zaidi ili kulipa madeni

Kenya kwa mara nyingine inatazamiwa kuchukua mkopo mpya wa KSh 780 bilioni wa Eurobond licha ya kurundikana kwa madeni yake.

Haya yameibuka kupitia kwa Shirika la Fedha Duniani (IMF), ambalo lilifichua kuwa serikali ya Rais Uhuru Kenyatta inapanga kuchukua mkopo mwingine wa kipindi cha mwaka mmoja unusu.

Kulingana na mpango wa mkopo ambao uliwasilishwa kwa IMF na Wizara ya Fedha, Kenya inapanga kukopa KSh 528 bilioni ambao una muda mrefu wa kulipa.

Mkopo mwingine wa KSh 253 bilioni ni wa kibiashara ambao una riba ya juu na kipindi kifupi cha kulipa.

IMF ilisema mpango huo unaruhusu Kenya kukopa zaidi ili kulipa madeni.

Kurefushwa kwa uwezo wa kukopaMnamo Januari, Hazina ya Kitaifa ilisema inapania kushinikiza bunge kuongezea Kenya mpaka mkopo kutoka KSh 9 trilioni hadi KSh 12 trilioni.

Hatua hiyo ni ya kuwezesha serikali kukopa zaidi ili kufadhili bajeti ya 2021/2022 imbayo inakumbana na uhaba wa fedha kwa sababu ya changamoto za mapato.

Takwimu za Benki Kuu ya Kenya zinaonyesha kufikia Novemba 2020, Kenya ilikuwa na madeni ya jumla ya KSh7.2 trilioni.

Hasira kuhusu mkopo wa IMF

Mnamo Ijumaa, Aprili 2, IMF iliidhinisha mkopo wa KSh 255 bilioni kwa Kenya huku janga la COVID-19 likikeketa.

IMF ilisema mkopo huo ni wa kusaidia Kenya kukabili COVID-19 na pia kupunguza madeni mengine.

Hata hivyo, Wakenya kwenye mitandao ya kijamii hawakufurahishwa na kuonyesha hasira zao kwenye ukurasa wa Facebook wa IMF kabla ya kuanzisha kampeni ya kufuta mkopo huo.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke