Waziri wa mambo ya ndani wa Kenya amesema kuwa nchi hiyo itatuma wajumbe wa tathmini hali nchini Haiti kabla ya kupeleka maafisa wa polisi kushughulikia ghasia za magenge huko.
"Kutakuwa na ziara nyingine za kabla ya kutuma polisi nchini Haiti na wadau mbalimbali kabla ya maafisa wetu kwenda huko," Waziri wa Mambo ya Ndani Kithure Kindiki aliiambia kamati ya bunge siku ya Alhamisi.
Mnamo Agosti, Kenya ilituma ujumbe wake wa kwanza wa kubaini ukweli nchini Haiti.
Bw Kindiki pia alisema kuwa maafisa hao wana vifaa vya kukabiliana na magenge ya Haiti kwani walitumwa ni kufanikiwa katika nchi kadhaa hapo awali, ikiwa ni pamoja na Namibia, Kambodia, iliyokuwa Yugoslavia, Bosnia na Herzegovina, Croatia na Sierra Leone.
Aliongeza kuwa maafisa wa polisi ni sehemu ya vikosi vya usalama vya Kenya vilivyotumwa hivi sasa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Somalia na Sudan Kusini.
Hata hivyo, amesema kuwa kupelekwa kwao Haiti kutafanyika baada kukidhivigezo vyote vya sheria, ikiwa ni pamoja na kuidhinishwa na bunge na seneti.
Wiki iliyopita, Umoja wa Mataifa uliidhinisha kupelekwa kwa maafisa wa polisi wa Kenya nchini Haiti lakini mahakama ya Kenya Jumatatu ilisimamisha kwa muda, hatua hiyo, ikisubiri uamuzi kubaini iwapo ni ya kikatiba au la.