Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kenya: Shule ya upili ya wasichana yafungwa baada ya 'ugonjwa wa ajabu'

Entrance To Eregi Girls High School In Kakamega County Kenya: Shule ya upili ya wasichana yafungwa baada ya 'ugonjwa wa ajabu'

Wed, 4 Oct 2023 Chanzo: Bbc

Wizara ya Elimu imefunga shule ya upili ya wasichana ya St Theresa's Eregi baada ya wanafunzi kadhaa kulazwa hospitalini kutokana na ‘’ugonjwa wa ajabu’’.

Hatua hii inachukuliwa huku Waziri wa Elimu Ezekiel Machogu akitarajiwa kutembelea taasisi hiyo baadaye leo.

Maafisa wa elimu katika Kaunti ya Kakamega waliamua kufunga kwa muda shule hiyo Jumatano baada ya wanafunzi kuibua ghasia.

Walikuwa wanataka kuruhusiwa kurudi nyumbani baada ya wanafunzi 90 kulazwa katika hospitali mbalimbali kufuatia mlipuko wa 'ugonjwa wa ajabu.'

Taarifa ya Serikali ya Kaunti ilisema kuwa Bodi ya Usimamizi, Maafisa wa Wizara ya Elimu na Tume ya Utumishi wa Walimu walifanya mashauriano kabla ya uamuzi kutolewa.

Hatahivyo wanafunzi wa kidato cha 4 wanaotarajiwa kuanza mitihani yao watasalia shuleni.

Mnamo Jumatano, maafisa wakuu wa kaunti wakiongozwa na Mwanachama wa Kamati Tendaji ya Kaunti ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bonface Okoth na mwenzake wa Huduma za Afya Benard Wesonga walitembelea shule hiyo.

Bw Okoth amesema sampuli za damu kutoka kwa wanafunzi walioathiriwa zimetumwa katika Taasisi ya Utafiti wa Matibabu ya Kenya (Kemri) jijini Nairobi na Kisumu kwa uchunguzi zaidi.

Chanzo: Bbc