Tue, 26 Mar 2024
Chanzo: Bbc
Familia za waathiriwa wa mauaji ya Shakahola yaliyotokana na dhehebu la funga hadi ufe zimekusanyika katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Malindi pwani ya Kenya kuchukua miili ya jamaa zao.
Miili 34 pekee ndiyo iliyolinganishwa na familia.
Mabaki hayo ni ya kwanza kukabidhiwa kwa familia zao baada ya takriban mwaka mmoja wa shughuli kibwa ya kuwatambua kwa kutumia DNA.
Mamia ya miili, ikiwa ni pamoja na ya watoto, ilifukuliwa kutoka kwenye makaburi ya halaiki ya kina kirefu yaliyogunduliwa mwezi Aprili mwaka jana katika msitu wa Shakahola.
Chanzo: Bbc