Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kenya: Kanisa Katoliki lawataka wabunge kuukataa mswada wa fedha wa 2024

Kenya: Kanisa Katoliki Lawataka Wabunge Kuukataa Mswada Wa Fedha Wa 2024 Kenya: Kanisa Katoliki lawataka wabunge kuukataa mswada wa fedha wa 2024

Mon, 17 Jun 2024 Chanzo: Bbc

Kanisa katoliki nchini Kenya limewataka wabunge kuuukataa mswada wa fedha wa mwaka 2024.

Akizungumza Jumapili Askofu kuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Nyeri Anthony Muheria amewataka wabunge kukataa Mswada wa Fedha kwa ujumla wake, akisema kuwa si haki kwa serikali kuweka hatua zisizofaa za ushuru kwa Wakenya ambao tayari wameelemewa na mizigo.

"Hii haihusu ni upande gani au ushawishi wa kisiasa uko upande gani; ni kuhusu wema na ustawi wa Wakenya. Hebu tupige kura na kutunga sheria kwa kile ambacho kinahudumia zaidi ya asilimia 80 ya nchi hii."

Muheria ameilaumu serikali kwa kukosa kukiri masaibu ambayo Wakenya wanakumbana nayo kutokana na hali mbaya ya kiuchumi iliyopo.

"Kudharau na kupuuza maoni ambayo yametolewa kunahitaji kutafakariwa. Serikali yetu na viongozi katika ngazi zote lazima wasikilize kile ambacho Wakenya wamesema," Muheria alisema.

Muheria aliitaka serikali kutafuta njia mbadala za kuongeza mapato badala ya kuweka mipango tofauti ya ushuru kwa Wakenya. “Uongozi wetu ni lazima ujitafakari ikiwa kweli uko katika utumishi wa wananchi au wanatimiza malengo yao wenyewe,” alisema. "Katika muktadha huu, Mswada wa Fedha unawaongezea Wakenya ushuru. Mipango hii isiyo na mpangilio, isiyounganishwa, isiyounganishwa ya kuongeza ushuru na kutafuta maeneo mapya ya ushuru inapaswa kuwa ya kimfumo zaidi."

"Tuongozwe na dhamiri, tusiruhusu chochote kingine kuathiri uamuzi wetu. Sikiliza wananchi na usahau migawanyiko ya kisiasa na shinikizo," Muheria alisema.

Kanisa Katoliki sasa limewataka wabunge kupigia kura Muswada wa Fedha wa 2024/2025 kwa uhuru, bila shinikizo kutoka kwa vyama vya kisiasa, huku mswada huo ukipangwa kuwasilishwa kwenye ukumbi wa Bunge siku ya Jumanne kufuatia mapumziko ya wiki moja.

Askofu Mkuu pia alielezea wasiwasi wake kuhusu wanasiasa kuendelea kutumiwa kwa makanisa kama majukwaa la mashambulizi ya maneno.

Chanzo: Bbc
Related Articles: