Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kenya Airways kumpeleka Mwamburi Mombasa kuondoa uchungu wa Stella

9d8acfa26c0a5926 Kenya Airways kumpeleka Mwamburi Mombasa kuondoa uchungu wa Stella

Tue, 18 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mnamo Mei 17, Wakenya waliungana na mwanamuziki Freshley Mwamburi kuadhimisha siku ambayo alitambua kuwa mpenzi wake Stella 'alikula fare'

- Mwaka huu, Mwamburi atakuwa na nafasi ya kupona kidonda hicho baada ya Shirika la Ndege, Kenya Airways kujitolea kumsafirisha Mombasa kujivinjari pamoja na mke wake

- Mapema Jumatatu, Mei 17, Wakenya walipakia memes za kuvunja mbavu kukumbuka namna Stella alivunja moyo wa Mwamburi

Mwanamuziki mkongwe Freshley Mwamburi atapata fursa ya kupona vidonda vyake vya kuvunjwa moyo na mpenzi wake Stella baada ya Shirika la Ndege, Kenya Airways kujitolea kumsafirisha Mombasa kwa likizo.

Mwamburi aliibuka maarufu kupitia wimbo wake wa Stella Wangu ambao unatokana na tukio la kweli ambapo muimbaji huyo alitumia pesa zake zote kumsafirisha mpenzi wake Japan lakini baadaye alimsaliti.

Huku ikitangaza kuwa Stella hataabiri ndege ya KQ Jumatatu, Mei 17, ishara kuwa amekula 'fare' ya mwanamuziki huyo, shirika hilo lilijitolea kumpeleka Mwamburi na mke wake Mombasa ili kupona uchungu huo.

"Tunaweza kuthibitisha kuwa Stella hatarudi nyumbani mwaka huu kwa sababu ya masharti ya usafiri.Tumeshindwa cha kusema. Hata hivyo, tungependa kutoa zawadi zake kupitia KQ Cargo. Na kwa Bwana FreshlyMwamburi, tunafurahia kuwa atasafiri nasi hadi Mombasa na mpenzi wake mpya kupunguza uchungu," ilisoma taarifa ya KQ.

Wengi walipongeza Kenya Airways kwa kutoa ofa hiyo wakisema anahitaji kupumua huku baadhi wakitania kuwa hawakuridhishwa na Stella kukosa kurejea nyumbani kwa Mwamburi.

Mapema Jumatatu, Mei 17, Wakenya walipakia memes za kuvunja mbavu kukumbuka namna Stella alivunja moyo wa Mwamburi.

Katika maadhimisho ya 29 ya siku hiyo ambayo Mwamburi hatawahi kusahau, Wakenya walijaa mitandaoni kupakia memes za kuvunja mbavu na video.

Baadhi walitania kuwa Stella ndiye aliibuka mwanamke wa kwanza "kula fare" ambayo alitumiwa na mpenzi wake huku akina dada wakitiana moyo kuendelea na mtindo huo.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke