Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kazi NI kupiga Ruto Tu: Naibu gavana amshambulia Mbunge Ngunjiri Wambugu

2af1a51513c1bfbc Kazi NI kupiga Ruto Tu: Naibu gavana amshambulia Mbunge Ngunjiri Wambugu

Sun, 23 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Naibu gavana wa Nyeri alikabili Ngunjiri Wambugu akisema kazi yake imekuwa ni kuwalima viongozi wengine badala ya kuchapa kazi

- Alimuonya kuwa yeye yuko tayari wakabiliane hata kwa mieleka iwapo hatakoma kukosoa siasa zake

- Duru zimearifu TUKO.co.ke kuwa tofauti za wawili hao ziliibuka baada ya ripoti kuwa huenda Karugu akawania kiti cha ubunge kinachoshikiliwa na Ngunjiri

Tofauti kali zimeibuka kati ya naibu gavana wa Nyeri Dkt Caroline Karugu na Mbunge wa Nyeri Mjini Ngunjiri Wambugu.

Karugu amesema Ngunjiri yuko na hulka za kuwalima kisiasa viongozi na anataka hilo likome mara moja.

Akiongea Jumamosi, Karugu alishangaa ni kwa nini mbunge huyo amekuwa akiendeleza siasa za kumlima naibu rais William Ruto.

"Ngunjiri amekuwa kazi yake ni kumtusi Ruto kila akiamka kana kwamba hiyo ndiyo kazi alichaguliwa kufanya," alisema Karugu.

e

Alisema yuko tayari kupambana na mbunge huyo wa Kieleweke kwa kuingilia siasa zake kila uchao.

"Ngunjiri aambiwe kina mama wa Nyeri hawawezi kuingiliwa vivi hivi,mimi niko tayari kupambana na yeye, anasema eti nachukua kiti chake . . . mimi hakuna kiti nimewahi kusimama.

"Aambiwe niko tayari, akitaka hata vita ya mwili tutapambana," alisema mwanasiasa huyo.

Karugu alikosoa mbunge huyo kutokana na njama yake ya kutaka Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i kuondolewa kazini.

Kupitia kwa ukurasa wake wa Facebook, Ngunjiri alisema atapanga karata ambapo wabunge wa ODM, UDA na Kieleweke wataungana na kumtimua Matiang'i.

"Sasa naskia eti huyo Ngunjiri ameanza kumlima Matiang'i eti kwa sababu alituma maafisa wa polisi wakuje hapa . . . mwambieni akuje polepole," alisema Karugu.

Ngunjiri amekuwa kwenye mstari wa mbele na kikosi chake cha Kieleweke kumlima DP Ruto na wandani wake wa Tangatanga.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemekem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke