Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kauli ya DP Ruto kuhusu vitisho vya Raila na Uhuru kwenye Urais 2022

46ccf9e795ea777d Kauli ya DP Ruto kuhusu vitisho vya Raila na Uhuru kwenye Urais 2022

Mon, 20 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Naibu Rais William Ruto kwa mara nyingine tena amewakashifu Rais Uhuru Kenyatta na kinara wa chama cha ODM Raila kwa kushirikiana na kutaka kuzima ndoto yake ya kuwa Rais.

Ruto amejutia kwamba watu aliosaidia kuingia madarakani ndio wao wanataka kumuangamiza kisiasaAkiashiria mpango wa BBI, Ruto alisema ilikuwa njama kwa Raila na Uhuru kuunda nafasi mpya serikalini kwa ajili ya manufaaa yao.

Naibu Rais William Ruto amesema mwaka wa 2007 alimfanyia kampeni Raila Odinga, mwaka wa 2013 na 2017 alimsaidia Uhuru kuwa Rais.

Ruto alisema licha ya kumfanyia kampeni Raila mwaka wa 2007 na kumsaidia Uhuru kuingia ikulu mwaka wa 2013 na 2017, bado hawa shukran ila wako mbioni kuhakikisha wanamangamiza kisiasa.

Akiashiria mikutano ambayo Uhuru na Raila wamekuwa wakifanya mara kwa mara, Ruto alisema hatatishwa na lolote na atahakikisha amekuwa Rais wa tano wa taifa hili.

"Mnajua vema kwamba nilimpigia kampeni Raila katika uchaguzi mkuu wa 2007, vile vile nikamsaidia rafiki wangu Uhuru kuwa rais mwaka wa 2013 na 2017 na kila mtu alishuhudia haya, lakini nashangaa hawa watu niliowasaidia hawataki kurudisha mkono badala yake wameungana wakidai kwamba sifai kuwa rais wa nchii hii.

" Nataka kuwambia kwamba hata mtoto wa single mum anaweza kuwa rais wa nchi hii," Alisema Ruto.

Hata hivyo, akiwa kwenye mkutano wa wanahabari mwezi Agosti, Uhuru alifutilia mbali madai kwamba amekuwa akiwachocha viongozi wengine dhidi ya kumpea Ruto fursa ya kuwa Rais.

" Yeye mwenyewe ndio tatizo, hafurahii wala kukumbatia mambo ambayo tunayafanya kwa manufaa ya Wakenya, sijawahi elewa ni kwa nini yeye hupinga kila kitu, mikutano ambayo mimi hufanya haijawahi husiana na uchaguzi mkuu wa 2022," Uhuru alisema.

Ruto pia alimkashifu Uhuru na Raila kwa kushinikiza kupitisha mpango wa BBI akidai kwamba ulinuia kuunda nafasi nono serikalini ili wajinufaishe wenyewe bila kujali mwananchi wa kawaida.

" Mnataka kutuambia eti mnafanyia katiba mabadiliko, ili mjiundie nafasi ya uwaziri mkuu na nafasi zingine mgawane miongoni mwenu, mnafikiria aje kuhusu hustler wengine, hayo hayawezi fanyika my friends," Alisema Ruto.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke