Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Katibu Mkuu wa UN 'asikitishwa sana' na hali ya Sudan

Antonio Guterres Mataifa Ukoloni Katibu Mkuu wa UN 'asikitishwa sana' na hali ya Sudan

Mon, 12 Aug 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Umoja wa Mataifa umelezea wasiwasi wake Jumapili kuhusu mapigano yanayoendelea kati ya Vikosi vya Jeshi la Sudan na wanamgambo wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) huko Darfur Kaskazini.

Farhan Haq msemaji wa Umoja wa Mataifa, amesema katika taarifa kwamba, Katibu Mkuu Antonio Guterres amesikitishwa sana na hali inayoendelea huko El Fasher, Darfur Kaskazini, ambako mapigano makali yameripotiwa kati ya Vikosi vya Jeshi la Sudan na wanamgambo wa RSF pamoja na wengine wanaohusika katika mapambano ya silaha."

Ameongeza kuwa mapigano haya yana madhara makubwa kwa raia.

Haq amesema mapigano hayo pia yatazidisha mahitaji ya kibinadamu ndani na karibu na El Fasher wakati ambapo hali ya njaa imethibitishwa katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Zamzam kusini mwa El Fasher na kuna uwezekano mkubwa katika maeneo mengine ya watu kuhama katika mji huo.

Msemaji huyo ameongeza kuwa: "Katibu Mkuu anatoa wito kwa pande zote kutii wajibu wao chini ya sheria ya kimataifa ya kibinadamu ya kulinda na kuruhusu kupita kwa usalama raia na kuwezesha ufikiaji wa haraka wa misaada ya kibinadamu bila vikwazo."

Akirejelea wito wake wa kusitishwa mara moja uhasama na usitishaji mapigano wa kudumu, Haq amesema kuwa Guterres pia amezitaka pande hizo kurejea kwenye mazungumzo ya kisiasa kama njia pekee ya kufikia suluhu iliyojadiliwa. Sudan

Sudan imekumbwa na vita kati ya jeshi, linaloongozwa na Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, ambaye ni mkuu wa Baraza la Mpito la Utawala, na kundi la RSF linaloongozwa na makamu wake wa zamani Mohamed Hamdan Daglo.

Kulingana na takwimu za Umoja wa Mataifa, takriban watu 12,260 wameuawa na zaidi ya 33,000 kujeruhiwa katika vita vilivyoanza Aprili 2023,

Mgogoro wa kibinadamu unaendelea kuwa mbaya zaidi kwani karibu watu milioni 6.8 wamekimbia makazi yao kutafuta usalama nchini Sudan au nchi jirani.

Jitihada za kieneo na kimataifa hadi sasa ziimeshindwa kukomesha mapigano hayo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live