Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Karata ya Uhuru: Mkutano wa Rais na Magavana wa Pwani wazua Hisia mseto

38292bda5f260216 Karata ya Uhuru: Mkutano wa Rais na Magavana wa Pwani wazua Hisia mseto

Thu, 25 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Rais Uhuru aliwasha ndimi za siasa baada ya kufanya kikao na magavana wa ukanda wa Pwani

- Mkutano huo ulionekana kama wa kupanga karata ya siasa za Pwani ambapo ODM imekuwa ikivuma

- Mbunge Oscar Sudi alisema lengo ni Rais kufadhili na kufufua vyama vya kimaeneo

Mkutano wa Rais Uhuru Kenyatta na magavana Hassan Joho wa Mombasa, Amason Kingi wa Kilifi na mwenzao wa Kwale Salim Mvurya umezua hisia mseto.

Wanne hao walikutana katika Ikulu ya Nairobi Jumatano Machi 25 katika kile kilitajwa kama kujadili maendeleo ya Pwani.

Baadhi ya viongozi wa kisiasa wamesema kikao hicho kilikuwa cha kupanga karata ya siasa za Pwani.

Mbunge wa Kapseret Oscar Sudi alisema Rais ana njama ya kufadhili chama cha kisiasa cha ukanda wa Pwani.



Kupitia kwa ukurasa wake wa Facebook, Sudi alisema Rais anataka kurudisha taifa katika siasa za ukabila.

"Nimekluwa nikiwaeleza Wakenya kuhusu karata za kisiasa za Uhuru Kenyatta. Sasa anataka kufadhili viongozi wa Pwani kuunda chama chao. Licha ya kuwa Gavana Mvurya huwa haungi mkono sera za kisiasa za Hassan Joho na Amason Kingi, Uhuru bado anataka awe kwenye mpango wa kuunda cha cha eneo hilo," aliandika Sudi.

Sudi alisema Rais amekuwa akifadhili kuundwa kwa vyama kama hivyo eneo la Magharibi na pia Kaskazini mwa Kenya.



"Ameshtuka kuwa siasa za Kenya sasa zimebadilika kutoka kwa ukabila na sasa anataka kucheza karata za kurudisha siasa hapo," alisema Sudi.

Gavana Joho na Kingi wamekuwa ni wandani wa kinara wa ODM Raila Odinga lakini hivi maajuzi wameanza kuimba wimbo wa chama cha Pwani.

Wakati wa ziara ya Raila eneo la Pwani hivui karibuni, Kingi alimwambia peupe kuwa wakati umefika kwa Pwani kuwa na chama chake.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke