Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kampuni ya 'Shell yabanwa vikali Nigeria uchafuzi a mazingira

Shell Kampuni Mafuta.png Kampuni ya 'Shell yabanwa vikali Nigeria uchafuzi a mazingira

Tue, 16 Apr 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Takriban mashirika arobaini ya kiraia, ikiwa ni pamoja na Amnesty International, yanapinga uuzaji wa mali za kampuni ya mafuta Shell hadi pale kampuni hii ya kimataifa itakaposafisha uchafuzi ulioachwa nyuma.

Mnamo mwezi wa Januari, kampuni hii ya Uholanzi na Uingereza ilitangaza kuwa imefikia makubaliano ya uuzaji wa mali yake ya Niger Delta kwa jumla ya hadi dola bilioni 2.4. Barua ya wazi iliyoomba mamlaka ya Nigeria kusitisha uuzaji huu ilichapishwa siku ya Jumatatu.

Mashirika yasiyo ya kiserikali yaliyotia saini barua hii ya wazi yanaomba serikali ya Nigeria "kukataa kibali cha kisheria cha uuzaji" wa mali ya Shell, ambayo ilifikia makubaliano mwezi Januari na muungano wa Renaissance Africa Energy, ambao unaleta pamoja makampuni manne ya Nigeria na kampuni ya Petrolin. .

Amnesty International inaelekeza kwenye mapungufu ya "kidhibiti na kisheria". Yaani kutokuwepo kwa utafiti wa mazingira na hesabu ya mali halisi inayouzwa, "ambayo inapaswa kutahadharisha juu ya uwezekano wa hali ya uharibifu wa mabomba ya mafuta na miundomsingi inayohusika na uvujaji mwingi", kulingana na Amnesty.

Kuna "hatari" kwamba Shell "inaweka mfukoni mamilioni ya dola (...) na kuwaacha waathiriwa wa uchafuzi wa mazingira bila msaada, na katika hali ya hatari kwa afya zao", kulingana na Amnesty.

"Uuzaji unapaswa kuidhinishwa tu wakati jamii zimeshauriwa kikamilifu, uchafuzi wa mazingira (...) kutathminiwa kikamilifu, na fedha za kutosha kuhakikisha gharama za kusafisha zilizowekwa na Shell", inaonyesha barua ya wazi iliyochapishwa siku ya Jumatatu.

Shell tayari imeagizwa kulipa euro milioni 15 kama fidia kwa wakulima wa Nigeria kutokana na uvujaji wa mafuta ambao ulichafua sana vijiji vitatu na maelfu ya wavuvi bado wanadai fidia kutoka kwa kampuni hiyo ya kimataifa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live