Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kampeni za uchaguzi Kenya na vioja vyake!

RTX7AQ4Y Scaled E1649664811845 Kampeni za uchaguzi Kenya na vioja vyake!

Mon, 30 May 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kampeni rasmi katika uchaguzi wa Kenya sasa inaendelea kabla ya upigaji kura mwezi Agosti.

Tayari, mapendekezo ghushi ya kuidhinishwa kwa wagombeaji wawili wakuu wa urais yanashirikiwa kote mtandaoni.

Tumekuwa tukiangalia baadhi ya machapisho na video za kupotosha za mitandao ya kijamii zinazosambazwa.

Rais Uhuru Kenyatta anastaafu baada ya mihula miwili ya uongozi.

Mmoja wa wanaotarajia kuchukua nafasi yake ni naibu wake, William Ruto.

Video imeibuka, ikidaiwa kumuonyesha aliyekuwa Rais wa Marekani, Barack Obama, akitangaza kumuunga mkono Bw Ruto.

Video hiyo hata hivyo imebadilishwa na haina uhusiano wowote na uchaguzi wa Kenya - Bw Obama hajaidhinisha mgombea yeyote.

Video hiyo iliyoshirikiwa na watu wengi imetayarishwa ili kumwonyesha Bw Obama akionyesha picha kubwa ya mgombeaji wake mteule, ikiwa na mabango ya uwongo kwenye skrini yanayoonyesha kuwa ni habari ya Habari za BBC, na ilichapishwa kwenye akaunti ya TikTok.

Maandishi yana hitilafu ya kisarufi na rangi za mabango hazilingani.

Video hiyo ya kweli, iliyotumika kama msingi wa hizo ghushi, ilirekodiwa katika Taasisi ya Smithsonian huko Washington mnamo 2018, ambapo Bw Obama alikuwa akionyesha picha yake mwenyewe

Chanzo: www.tanzaniaweb.live