Wed, 14 Apr 2021
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke
Wakazi wa kaunti tano zilizofungwa na Rais Uhuru Kenyatta kwa kuwa na idadi kubwa ya maambukizi ya coronavirus watasalia na kafyu hadi mwisho wa Mei.
Waziri Fred Matiang'i alisema kafyu ya kutotoka nje ya kaunti hizo tano za Nakuru, Nairobi, Kiambu, Kijiado na Machakos itasalia.
Wakati wa kuweka kafyu hiyo, Rais alitangaza wakazi wawe wakifika nyumbani kabla ya saa mbili usiku na kulala hadi saa kumi na moja asubuhi.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke