Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jumuiya ya Kimataifa yalaumiwa mgogoro wa DRC

Image 83.png Jumuiya ya Kimataifa yalaumiwa mgogoro wa DRC

Wed, 7 Dec 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Serikali ya Rwanda, imeishutumu Jumuiya ya kimataifa kwa kuchochea mgogoro wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC, baada ya Marekani kuishinikiza Rwanda kusitisha uungaji mkono kwa waasi katika eneo hilo.

Vincent Biruta jana jioni alitowa taarifa akisema mwelekeo usiofaa na unaopotosha unaoonyeshwa na jumuiya ya Kimataifa unaendelea kuongeza tatizo, uingiliaji kutoka nchi za nje na matamshi ya kuamrisha ni mambo yanayohujumu jitihada za kikanda za usuluhishi.

Juhudi za kutafuta amani zinazowahusisha maafisa wa jumuiya ya Afrika Mashariki na makundi mbali mbali ya waasi wa Kongo zinaendelea huko Nairobi Kenya na Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda pia anasema wasiwasi wa nchi yake unapaswa kushughulikiwa.

Serikali ya Rwanda, mara kadhaa imekuwa ikiilaumu Serikali ya Kongo kuhusu mgogoro wa mashariki mwa nchi yake, na kuishutumu jumuiya ya kimataifa kwa kufumbia macho suala la DRC kuwaunga mkono waasi wa FDLR.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live