Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jubilee iliundwa kusaidia Ruto 2022, Murathe Asema

Be282e1fe38811f0 Jubilee iliundwa kusaidia Ruto 2022, Murathe Asema

Tue, 20 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Chama cha Jubilee kiliundwa ili kufikia 2017 kimsaidia DP Ruto kusaka kura kwa mujibu wa Murathe

- Akiongea na runinga ya Inooro, alisema tatizo la DP lilikuwa kukimbilia Ikulu badala ya kusubiri Rais aondoke

- Alisema kwa sasa kuna karata kubwa inachezwa ili kuhakikisha kuwa DP hataingia Ikulu ifikapo 2022

Naibu Mwenyekiti wa Jubilee David Murathe amesema chama cha Jubilee kiliundwa ili kumsaidia Naibu Rais William Ruto kwenye uchaguzi wa 2022.

Murathe alisema Uhuru Kenyatta na Ruto waliungana 2013 walipoleta pamoja vyama vyao vya URP na TNA lakini 2017 wakaamua kuunda chama kimo cha Jubilee kwa ajili ya 2022.

"Ilikuwa ni njama ya kuunganisha Mt Kenya na makabila mengine ili iwe rahisi kwake 2022. Ilikuwa imeundwa ili kusaidia naibu rais," alisema Murathe.

Alisema tatizo kubwa kati ya Rais Uhuru na Ruto zilitokea baada ya uchaguzi wa 2017 alipotaka usemi zaidi serikalini.



"Alikuwa anataka apewe funguo za ghala ili aweze kupata michuzi ya 2022. Wakati Rais alikataa, hapo ndipo alikasirika," Murathe alisema wakati wa mahojiano na runinga ya Inooro.

Murathe alisema kuna kundi la watu ambao watahakikisha kuwa DP Ruto hajaingia Ikulu kumrithi Rais Uhuru.

"Wao husema kama hivi ndivyo alivyo akiwa nambari mbili, itakuwaje akiwa nambari moja? Wameamua watafanya kila liwezekalo kumzuia kuchukua hatamu za uongozi," alisema.



Alifichua kuwa kutakuwa na miungano mbalimbali ambayo baadaye itahakikisha kuna wimbi la kummaliza DP Ruto.

"Miungano imeanza. Kama vile ilifanyika 2002, hii miungano kama One Kenya Movement mimi naona itafika mahali ikuje pamoja. Hii mipango itahakikisha hajaingia Ikulu," alisema Murathe.

Murathe alisema yeye ombi lake ni Raila Odinga apatiwe urais 2022 kama zawadi ya kufanya handisheki na Rais.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke