Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jubilee haiwezi kuungana na ODM, katibu Raphael Tuju Asema

B5536e872eaac9b9 Jubilee haiwezi kuungana na ODM, katibu Raphael Tuju Asema

Thu, 22 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Tuju alikanusha madai kuwa ODM na Jubilee zinapanga kuungana kwa ajili ya uchaguzi wa 2022Alisema kilichopo kwa sasa ni urafiki tu kati ya vyama hivyo viwili kutokana na mkataba wa handishekiDP na wandani wake wamekuwa wakisema kuna njama ya vyama hivyo viwili kuungana na hivyo kuwataka wafuasi wao kuingia UDAKatibu wa Jubilee Rapahel Tuju amepuuza madai kuwa chama chake kina mipango ya kuungana na ODM.

Akiongea na kituo kimoja cha runinga humu nchini, Tuju alipuuza madai hayo akisema kilichopo ni mkataba wa urafiki tu.

Alisema ODM imekuwa kiungo muhimu katika uongozi wa Jubilee kwani wamekuwa wakisaidia kupitisha miswaada mbali mbali.

“Watu wanaona tumeketi na ODM tukiongea kwa sababu ni marafiki wetu alafu wanaanza kusema kuna mipango ya kuungana. Hata hawajui maana ya vyama kuungana, kilichopo ni mwafaka wa makubaliano kati ya ODM na Jubilee,” alisema Tuju.



Read also

Mkutano wa Mudavadi, Kalonzo na Moi Wadhihirisha Kifo cha NASA



Tuju alisema ni kosa kwa wapinzani wao wa kisiasa kusema kuna muungano kati ya Jubilee na ODM ilhali hawazungumzii mwafaka kati ya chama chake na Wiper.

“Kwani ni ODM tu ambapo wanasema kuna muungano. Tuko na mwafaka pia na chama cha Wiper na hawasemi huo ni muungano,” alisema Tuju.

Alisema kwa sasa ODM ni wandani wa Jubilee kutokana na mkataba wa handisheki kati ya Rais Uhuru Kenyatta na kinara wa ODM Raila Odinga.

Naibu Rais William Ruto amekuwa katika mstari wa mbele kukashifu uongozi wa Jubilee akisema kuna mipango ya kuungana na Jubilee.

Akiongea mwezi Juni wakati wa ziara katika kaunti ya Nakuru, aliwataka wafuasi wake kujiandaa kuingia chama kipya cha UDA akisema Jubilee imetekwa na ODM.

“Kuna watu wanataka eti nyinyi mkaungane na ule mtu wa kitendawili. Hiyo inawezekana kweli? Eti nyinyi sasa muwe ni watu ya kuskiza kitendawili?” alisema Ruto.



Read also

NIS Ilionya Rais Uhuru Kwamba Jubilee Itabwagwa na UDA Kiambaa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke