Kikundi cha wanajeshi waliomwondoa Rais wa Guinea Alpha Condé mamlakani September 5, 2021 wameamuru baraza la mawaziri la nchi hiyo kuhudhuria mkutano wa lazima Jumatatu.
Taarifa hii imetolewa kupitia televisheni ya Taifa nchini humo, na kusistiza kuwa wale ambao watakataa kuhudhuria mkutano huo watachukuliwa kuwa waasi, taarifa kwenye Televisheni ya serikali imesema.
Hata hivyo, Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika, na shirika la kikanda la Ecowas wamelaani mapinduzi hayo na kutoa wito wa kurejeshwa kwa utawala wa raia.
Mkuu wa vikosi maalum vya nchi hiyo, Kanali Mamady Doumbouya, amesema wanajeshi wake wamechukua madaraka kwa sababu wanataka kumaliza ufisadi uliokithiri na usimamizi mbaya