Jeshi la Kongo limewashutumu waasi wa M23 kwa kuwaua takriban raia 50 katika mji wa mashariki wa Kishishe.
Haya yanajiri huku kukiwa na taarifa za mauaji ya watu wengi kufuatia kuanza tena kwa mapigano, huku usitishaji mapigano uliokubaliwa wiki iliyopita ukionekana kuporomoka.
Kundi hilo la waasi limekanusha madai dhidi yao kuwa "hazina msingi", likisema kuwa halijawahi kuwalenga raia
Maelfu ya watu wanakimbia mapigano kati ya waasi, vikosi vya serikali na wanamgambo washirika katika maeneo tofauti ya jimbo la Kivu Kaskazini.
Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zilikubaliana katika mazungumzo nchini Angola kwamba usitishaji vita utaanza kutekelezwa Ijumaa iliyopita.
M23 walisema mapatano hayo hayakuwahusu kwani hawakualikwa kwenye mazungumzo hayo. Rwanda inakanusha madai kwamba inaunga mkono M23