Tue, 7 Sep 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkuu wa Kikosi Maalum cha Jeshi kilichompindua Rais Alpha Conde amesema, Maafisa wa Serikali ya Guinea sasa hawatoruhusiwa kusafiri nje ya Nchi.
Kanali Mamady Doumbouya , pia amekiambia Kikao cha Mawaziri wa Conde akiwemo Waziri Mkuu na Maafisa wengine wakuu Serikalini kwamba warudishe Magari ya Serikali waliokuwa wakiyatumia katika kutekeleza majukumu yao kipindi cha utawala uliopita.
Mapinduzi katika Nchi hiyo yenye utajiri mkubwa wa Madini ya Bauxite ambayo hutengeneza Chuma cha Pua, yamesababisha bei ya chuma hicho kuongezeka kwa kiasi ambacho hakijawahi kushuhudiwa katika Miaka 10.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live