Sun, 25 Feb 2024
Chanzo: Bbc
Makumi ya wanajeshi wa Somalia wamewasili nchini Kenya kwa mazoezi ya kijeshi yatakayoshirikisha nchi kadhaa za Afrika.
Makomando waliopewa mafunzo maalum ya Danab wa Somalia watakuwa wa kwanza kushiriki katika mazoezi ya kijeshi nje ya nchi hiyo tangu kuangushwa kwa serikali ya Mohamed Siad Barre mwaka 1991.
Kamanda wa jeshi la Somalia, Jenerali Ibrahim Sheikh Muhyiddin, amelitaka jeshi la Somalia linaloshiriki mazoezi hayo kuonyesha vipaji miongoni mwa mamia ya wanajeshi wanaoshiriki zoezi hilo, na kuleta sifa kwa taifa la Somalia.
Chanzo: Bbc