Jeshi la Mapinduzi nchini Guinea, limewaachia huru Wanasiasa wa upinzani zaidi ya 79 waliokuwa wakitumikia vifungo katika mji wa Conakry nchini humo.
Hatua hii inakuja wakati Jumuiya ya nchi za Afrika Magharibi ikiwa katika mchakato wa kukutana kujadili mwenendo wa kidemokrasia na usalama nchini humo pamoja na kushinikiza kuachiwa kwa Rais Aplha Conde aliyetolewa madaraka na jeshi hilo Septemba 05, 2021.
Mwanasheria anaye shughulikia kesi za viongozi hao, amethibitisha taarifa hii kwa kusema kuwa tayari washitakiwa 79 wamesharuhusiwa kutoka mara baada ya kufanya mazungumzo na uongozi wa jeshi hilo.
Hata hivyo Jeshi hilo liliitaka Mahakama kuhakikisha inaharakisha upatikanaji wa haki ikiwa ni pamoja na kuwaachia huru wanasiasa hao ambao kwa mujibu wao ni wameshtakiwa kinyume cha sheria