Mwili wa mwanamume mmoja ulitolewa kwenye kifusi nchini Afrika Kusini katika Jengo linaloendelea kujengwa ambalo liliporomoka Jumatatu hii, Mei 6 mchana, huko George Kusini mwa nchi hiyo.
Polisi wamesema kuwa Wafanyakazi 47 bado wamekwama kwenye kifusi, shughuli za uokozi zikiendelea na kuongeza kuwa uchunguzi umefunguliwa kuhusu tukio hilo.
Kwenye video za kamera za uchunguzi, Jengo la ghorofa nne lilionekana likiporomoka kwa sekunde, na kuacha uwanja wa vifusi tu.
Operesheni imefanyika usiku kucha, ikiwa ni pamoja kutumia mbwa wa kunusa kwa ajili ya kuwaokoa watu walionasa kwenye kifusi.
Hadi kufikia sasa haijajulikana sababu ya kuporomoka kwa Jengo hilo ambalo lilikuwa linajengwa kwa ajili ya makazi ya watu.