Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jengo la ghorofa nne laporomoka

Infinity Building Jengo la ghorofa nne laporomoka

Thu, 11 Aug 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Jumba moja liliporomoka katika eneo la Infinity eneo la Mwiki Estate, eneo la Kasarani jijini Nairobi, jana Jumatano jioni.

Timu ya St John Ambulance iliwahi kufika katika eneo la tukio katika juhudi za uokoaji.

Hakuna waathiriwa wowote ambao wameripotiwa lakini inasadikiwa huenda kukawa na watu walionasa ndani ya jengo hilo.

"Timu zetu za kukabiliana na dharura zikikimbilia eneo la tukio. Taarifa zaidi zitafuata hivi punde," St John Ambulance ilisema kupitia Twitter.

Jengo la ghorofa nne lililoporomoka lilikuwa ni nyumba ya kupangisha ambapo Polisi wamesema kuwa shughuli za uokoaji bado zinaendelea. Kikosi cha Kenya Red Cross pia kimeonekana katika eneo la tukio.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live