Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jaribio la Jeshi kupindua serikali ya Sudan latibuka, maafisa 40 wakamatwa

2739cee5a8674084 Jaribio la Jeshi kupindua serikali ya Sudan latibuka, maafisa 40 wakamatwa

Tue, 21 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Serikali ya Sudan imebainisha kwamba kumekuwa na jaribio la jeshi kupindua mamlaka nchini humo.

Shughuli ya kuwahoji maafisa 40 waliokamatwa na wanaoshukiwa kupanga mapinduzi hayo itaanza muda mfupi ujao.

Jaribio hilo la mapinduzi ya serikali lilishuhudiwa mnamo Jumanne, Septemba 21, na hatua zinachukuliwa kudhibiti hali hiyoKulikuwa na jaribio la kuchukua jengo ambalo lina vyombo vya habari vya serikali.

Kulingana na vyombo vya habari vya serikali nchini humo, jaribio hilo la mapinduzi ya serikali lilishuhudiwa mnamo Jumanne, Septemba 21, na hatua zinachukuliwa kudhibiti hali hiyo.

"Kumekuwa na jaribio la mapinduzi lililoshindwa, watu wanapaswa kukabiliana nalo," Shirika la habari la AFP lilinukuu moja ya duru nchini humo.

Inaripotiwa kwamba kulikuwa na jaribio la kuchukua jengo ambalo lina vyombo vya habari vya serikali, maafisa wakuu serikalini walifichua.

Msemaji wa serikali nchini Sudan amesema kuwa shughuli ya kuwahoji maafisa 40 waliokamatwa na wanaoshukiwa kupanga mapinduzi hayo itaanza muda mfupi ujao.

Kufuatia tukio hilo, wanajeshi wa Sudan wamezingira mji mkuu wa Khartoum huku taarifa kamili ya jeshi ikitazamiwa kutolewa baadaye hii leo Jumanne, Septemba 21.

Wanajeshi wa Guinea Wapindua Serikali na Kumkamata Rais Tukio hilo la Sudan linakujia yapata wiki chache baada ya lingine kushuhudiwa nchini Guinea.

Hii ni baada ya video kusambaa ikimuonyesha Rais wa Alpha Condé mikononi mwa wanajeshi wa taifa hilo ambao walisema wamepindua serikali.

Umoja wa Afrika(AU) ulilaani mapinduzi hayo ya Guinea na kulitaka jeshi la taifa hilo kumuachilia huru Rais Alpha Conde haraka iwezekanavyo.

Mnamo Jumapili, Septemba 19, watawala wa kijeshi nchini Guinea jana wameondoa uwezekano wa kumruhusu rais wa zamani anaeshikiliwa Alpha Conde kwenda uhamishoni, na kusema mchakato wa mpito kuelekea utawala wa raia utafanyika kulingana na matakwa ya raia wa nchi hiyo.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke