Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jamaa asafiri kutoka Marekani kumuoa mama mwenye watoto 10

252adf69e7296db9 Jamaa asafiri kutoka Marekani kumuoa mama mwenye watoto 10

Wed, 28 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Janet na mume wake walifunga pingu za maisha Disemba 2020 na walikuwa hawajawahi kukutana kabla ya siku hiyo spesheli

- Wawili hao walijuana baada ya video ya Janet kusambaa na wakati mwanamume huyo aliitazama akiwa Marekani, aliguswa sana

- Walianza kuwasiliana kupitia simu na hata mwanamume huyo kumposa kisha mipango ya harusi ilianza akiwa bado ughaibuni

- Siku ya harusi hiyo, ndege ya bwana harusi ilitua na kukutana na mke wake kwa mara ya kwanza

- Mama huyo ambaye alikuwa kahaba zamani ana 10 kutoka kwa wanaume tofauti

Jaribu kuweka taswira ya picha ya siku ya harusi yako kila kitu kimeandaliwa lakini una wasiwasi kwa sababu haujawahi kukutana na mwanamume ambaye anataka kukuoa.

Kando na hali hiyo kuonekna nadhimu, hii ni hadthi ya Janet, ambaye alikutana na mume wake Jackson siku ya harusi yao.

Akizungumza kwenye mahojiano na Afrimax, Janet alisema mume wake ambaye alikuwa anaishi Marekani, alimjua baada ya video yake kusambaa akisimilia namna alivyowacha ukahaba na kuokoka.

Alisema video hiyo ilimfanya kudhalilishwa hususan baada ya kuchapishwa bila ruhusa yake lakini ilimvutia mwanamume mmoja ambaye aliguswa na ushuhuda wake.

"Aliona ushuhuda wangu na aliguswa. Alihisi kwamba tunatakiwa kuishi pamoja milele," alisema.

Alitafuta nambari zake za simu akiwa Marekani na baada ya kuzipata alimpgia na kuanza urafiki na kisha wakaishia kuwa wapenzi.

Walikuwa wakizungumza kila siku na wakati mapenzi yao yalikolea na kuwa dhabiti, alimposa kupitia simu na kisha punde si punde mipango ya harusi ilianza.

Jamaa huyo hakubabaishwa na ukweli kuwa mama huyo ana watoto 10 ambao aliwaza akiwa kahaba.

Badala ya kubabaishwa na maisha yake ya zamani, alichagua kumuoa mwanamke ambaye alikuwa anajaribu kuishi maisha mapya.

Janet alisema alikumbana na pingamizi kutoka kwa kanisa lake kwa kumuona kama mwenye dhambi kubwa zaidi kufanya harusi lakini alikumbatiwa na kanisa lingine ambalo liliidhinisha ndoa yake Disemba 2020.

Siku ya harusi hiyo, ndege ya bwana harusi ilitua na kukutana na mke wake kwa mara ya kwanza na kisha wawili hao walibadilishana viapo vya ndoa.

Baada ya kubadilishana viapo vya ndoa, wapenzi hao walikaa pamoja kwa wiki kadhaa kabla ya mwanamume huyo kurejea Marekani na kuanza mipango ya Janet kuhamia nchini humo.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke