Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jamaa apatikana ameaga dunia baada ya kulala na mwanamke

7d4efa949e822bc6 Jamaa apatikana ameaga dunia baada ya kulala na mwanamke

Sat, 10 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mwanamume huyo ambaye alikuwa amekodi chumba hicho mnamo Ijumaa, Aprili 9 alipatikana ameaga dunia saa tatu usiku na keyateka wa hoteli hiyo

- Kulingana na mhudumu huyo, Harrison Murimi, marehemu alikilipia chumba hicho saa sababu adhuhuri kisha baadaye mwanamke ambaye hatjatambulika alijiunga naye kabla ya kutoweka

- Maafisa wa polisi wameanzisha msako dhidi ya mwanamke huyo na kuwataka wamiliki wa hoteli katika mkoa huo kuhakikisha wanarekodi maelezo ya wateja wao wote

Jamaa mwenye umri wa makamo amepatikana ameaga dunia katika hoteli moja Kirinyaga baada ya kujivinjari usiku kutwa na mwanamke asiyejulikana.

Mwanamume huyo ambaye alikuwa amekodi chumba hicho mnamo Ijumaa, Aprili 9 alipatikana ameaga dunia saa tatu usiku na keyateka wa hoteli hiyo.

Mwenyekiti wa Kiagio Nyumba Kumi Daniel Kangangi alithibitisha kisa hicho.

"Keyateka ni kakangu, alipinipia simu niliwaarifu maafisa wa polisi wa kituo cha Kagio," Kangangio aliiambia Citizen TV.

Kulingana na keyateka, Harrison Murimi, marehemu alikuwa amepanga chumba hicho karibu saa saba mchana na baadaye mwanamke fulani ambaye alitoweka baaye alikuja kumuona.

“Tunalipisha KSh 300 tu, lakini haturekodi maelezo ya mtu kibinafsi. Kitu pekee ninachoweza kukumbuka ni kwamba mwanamke huyo alikuwa na mavazi mekundu, ” Murimi alifunua.

Maafisa wa polisi wameanzisha msako dhidi ya mwanamke huyo na kuwauliza wamiliki wa hoteli katika mkoa huo kuhakikisha wanarekodi maelezo yote ya wateja wao.

Mwili wa marehemu ulipelekwa katika makafani ya Kutus Funeral Home.

Mnamo Februari, mwanamume mwenye umri wa miaka 58 pia aliaga dunia baada ya kulala katika lojing'i moja Nyandarua.

Kulingana na ripoti ya polisi, Edith Wairimu Mwangi alimkuta marehemu chumbani akipumua kwa ugumu akiwa Heshima Lodge Ol Kalou.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 55 kisha alikimbilia Kituo cha Polisi cha Ol Kalou kuripoti kisa hicho ambapo polisi walikimbia eneo la tukio wakiandamana na maafisa kutoka Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI).

Alikimbizwa katika hospitali ya JM Kariuki ambapo alikuwa tayari ameaga dunia.

"Marehemu alipatikana na mpira wa kondomu kwenye uume wake. Maafisa wa upelelezi walidaiid kwa kina eneo la tukio kabla y kuupeleka mwili wake kwenye makafani kufanyiwa upasuaji," ripoti ya polisi ilisema.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke