Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jamaa anaswa kwenye video akila sacramenti kwa soda wakati wa ibada kanisani

Ab43da048b37c6c0 Jamaa anaswa kwenye video akila sacramenti kwa soda wakati wa ibada kanisani

Tue, 15 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Jamaa mmoja amezua mshawasha mtandaoni kufuatia matendo yake ya ajabu wakati wa ibada kanisaniMwanamume huyo asiyejulikana alikula sacramenti kwa soda ambayo alikuwa amebeba kanisaniVideo hiyo iliyosambaa imeibua hisia mseto miongoni mwa wanamtandao huku wengi wakitania kwamba hana makosa kwani alikuwa katika nyumba ya baba yake

Jamaa mmoja ameibua msisimko mtandaoni baada ya video kuibuka ikimuonyesha akifanya matendo ya ajabu wakati wa ibada kanisani.

Mwanamume huyo asiyejulikana alikula sacramenti kwa soda ambayo alikuwa amebeba kanisani.

Katika video ambayo ilipachikwa kwenye Instagram na Instablog9ja, jamaa huyo anaonekana kutojali endapo mtu anamuangalia akinywa soda hiyo akiwa amesimama.

Video hiyo iliyosambaa imeibua hisia mseto miongoni mwa wanamtandao huku wengi wakitania kwamba hana makosa kwani alikuwa katika nyumba ya baba yake.

@adorablekween aliandika: "Unaweza tambua kile anapitia. pengine ana vidonda vya tumbo ama huenda anatakiwa kumeza dawa fulani.Kwani lazima tuposti video za kila kitu mtandaoni."

@andyblayz said: ''Wakati makanisa yanakosa kufungwa kwa wakati ! Hiki ndicho kitatokea..."

@dessie_benz alisema: "Katika haya maisha siwezi kujiua.Kweli Yesu alimfia jamaa huyu."

Kwingineko, shujaa wa maombi kutoka nchini Ugandan ameaga dunia baada ya kugongwa na mti unaoshukiwa kuwa na mapepo.

Jimmy Obong, mwenye umri miaka 35, alifariki akiwa pamoja na mashujaa wenzake wa maombi wakimuombea John Okodi katika kijiji cha Tecwao, Alebtong.

Ben Ogwang alikuwa ameandaa hafla ya maombi kwa jamaa yake mgonjwa aliyetambuliwa kama John Okodi, ambapo alimualika Obong kuwa miongoni mwao.

Wakati wa maombi hayo mwanamke mmoja alipagawa na mapepo kisha anaripotiwa kuwaelekeza watu katika mti ambao ulidaiwa kuwa na mapepo yanayohangaisha familia ya Okodi.

Kisha baadaye waliamua kukata mti huo ambao ulimuangukia Obong ambaye alifariki papo hapo.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke