Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jalang'o akana madai kwamba hula "Lunch" inayomgharimu KSh 50,000 kila siku

0fgjhs67qhelm2s32 Jalang'o akana madai kwamba hula "Lunch" inayomgharimu KSh 50,000 kila siku

Fri, 23 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mtangazaji Jalang'o amezungumzia madai kwamba chakula chake cha mchana humgharimu KSh 50,000 kila siku Kulingana na Jalang'o madai hayo yalitolewa kupitia kwenye akaunti feki yenye majina yake mtandaoni FacebookMashabiki wake wamempongeza Jalang'o kwa kufafanua madai hayoMchekeshaji Felix Odiwour almaarufu Jalang'o amefutilia mbali madai kwamba yeye hununua chakula cha mchana kinachomgharimu KSh 50,000 kila siku.

Jalang'o alisema kuna mtu ameunda akaunti feki kwenye mtandao wa Facebook kwa kutumia jina lake ambaye amekuwa akiwahadaa wanamitandao kuhusu aina ya maisha anayoishi.

" Mimi hula lunch inayonigharimu KSh 50, 000 kila siku," posti hiyo ilisoma.

Akionekana kushangazwa na madai hayo, Jalang'o alijibu," Kwani pia nitakuwa nakula sahani na viti?, wapendwa jitahadhari na akaunti hii, hawa ni wakora wanaotumia jina langu kuwaibia Wakenya."



Read also

Ruto Apokonya Uhuru 'Mali' Yake na Habari Zingine za Kusisimua Wiki Hii

Mashabiki walipongeza Jalang'o kwa kujitokea na kufafanua madai hayo, wengi tayari walikuwa wamemkashifu kwa kuharibu kiwango hicho cha pesa kwa chakula siku moja tu.

Baadhi ya maoni ya mashabiki;

@HR Scholar alisema:

" Nilikuwa nashanga iwapo mbunge mtarajiwa wa Langata ako salama, hata hivyo bado tunakungoja."

@Muhanji Wycliffe alisema:

" Nilikuwa nashangaa sana lakini asante kwa kutufafanulia, tumekuelewa sasa."

@Okong'o Isaiah alisema:

" Nilishtuka sana, nilidhani ulikuwa ukila pia meza viti na gesi.

@PS Edeke said:

Iwapo unakumbuka wakati ulikuwa uking'ang'ana pale Jicho Four Production, na sai umefanikiwa, singeamini ni wewe unaharibu hivyo pesa."

Juma James Alisema:

"Watu waliokuwa wakikukashifu hawakujua hiyo ni akaunti feki."

Read: ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke



Read also

Magazeti Alhamisi, Julai 22: Ruto Kukumbana na Vita vya Umiliki wa UDA
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke