Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jaji Mkuu mteule Martha Koome apuzilia madai kwamba anawachukia wanaume

D19bddb59bfd3ffc Jaji Mkuu mteule Martha Koome apuzilia madai kwamba anawachukia wanaume

Fri, 14 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Wakati wa kupigwa msasa wa nafasi ya Jaji Mkuu, mbunge wa Suna Junet Mohammed alimuuliza mteule Jaji Martha Koome swali linaloonekana kuwa la kutatanisha

- Kulingana naye, kulikuwepo na fununu kwamba Jaji Koome aliwachukia wanaume

- Koome alijibu kwa kufichua kwamba maamuzi yake mara nyingi yamewapendelea wanawake na kwamba ameolewa ka miaka 35

Huku zoezi la kumsaka Jaji Mkuu wa taifa likiendelea, suala la jinsi ya kike na familia limeibuka tena.

Kwa kuzingatia ushawishi ambao Mahakama inao katika kutunga na kutafsiri sheria za nchi, maswala yaliyogusa jinsia yalizungumziwa kwa kina.

Hivi ndivyo ilivyokuwa wakati Mbunge wa Suna Junet Mohammed alipouliza swali linaloonekana kuwa la kutatanisha kwa Jaji Mkuu mteule Martha Koome.

"Kuna fununu kwamba wewe ni unawachukia wanaume. Tafadhali fafanua hilo," aliuliza Junet.

"Ninafuata maagizo ya katiba, ya sheria hiyo. Siwezi kamwe kufanya kazi nje ya katiba. Siwachukii wanaume. Kwa kweli, nimeolewa kwa miaka 35 iliyopita," alijibu.

Pia alichukua fursa ya kuzungumzia suala ambalo wazazi wengi ambao wamesome wamekuwa wakikabiliana nalo; kusawazisha elimu na familia wakati huo huo.

"Ninajivunia kuwa nilihitimu na binti. Pia nilihitimu na mume ambaye amebaki mpenzi wangu mpendwa kwa miaka yote hii," aliendelea.

Koome alisisitiza kwamba familia huunda msingi wa jamii na kulinda taasisi hiyo inalinda kila mtu kwa sababu washiriki wanajikita katika kutafuta maisha halali bila hofu.

"Ikiwa imeidhinishwa, ninatumahi kutumia mamlaka nitakayokuwa nayo kama Jaji Mkuu kuzungumza na familia ambazo tunahitaji kulea, kuwezesha, na kulinda watoto wetu," alisema Koome.

Koome alifafanua kuwa mapenzi yake kwa familia na jamii yatawafanya Wakenya kujisikia salama ikiwa atapewa nafasi hiyo.

Licha ya kwamba Koome alimjibu Junet kwa utulivu na ufasaha, swali lake lilidhihirisha wazi dhana potovu ulimwenguni kwamba wanawake wakiwa uongozini watawachukia wanaume.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke