Mon, 20 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Idadi ya waliofariki kutokana na Kimbunga #Freddy kilichodumu kwa takriban mwezi mmoja, imeongezeka hadi 522, kulingana na mamlaka nchini Malawi, Msumbiji na Madagascar.
Shirika la hali ya hewa Duniani( WMO) linasema kuna uwezekano kuwa CycloneFreddy, kilichoanza Mwezi Februari, 2023 na kusababisha maelfu ya watu kubaki bila makazi, ndicho kirefu zaidi kuwahi kurekodiwa katika historia.
Inaelezwa kuwa idadi ya vifo katika Nchi za Malawi na Mozambique inatarajiwa kuendelea kuongezeka.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live